Fahamu Uhusiano wa Tanzania na Urusi ulivyoanza miaka ya 60

06Mar 2024
Na Mwandishi Wetu
Dar es Salaam
Nipashe
Fahamu Uhusiano wa Tanzania na Urusi ulivyoanza miaka ya 60

Uhusiano thabiti kati ya Urusi na Tanzania, ulioanzia miaka ya 1960 mapema wakati Tanzania ilipojitenga na utawala wa ukoloni wa Uingereza, unatoa ushuhuda wa kuvutia kuhusu uhusiano wa kidiplomasia na urafiki uliopo kati ya mataifa haya mawili...

...ambayo umekuwa ukistawi kwa zaidi ya miongo sita iliyopita.

 

Wakati wa enzi ya Vita Baridi, Tanzania chini ya uongozi wa Julius Nyerere, ilifuata sera ya kutofungamana na upande wowote, ikisaka msaada kutoka nchi za Magharibi na Mashariki. Umoja wa Kisovieti, sasa Urusi, uliiona Tanzania kama Mshirika Mkakamavu Barani Afrika na kutoa msaada katika sekta mbalimbali, ikiwa ni pamoja na miundombinu, elimu, na ulinzi.

 

Ushirikiano uliongezeka kutokana na mwelekeo wa kisoshalisti wa Tanzania na msimamo wake dhidi ya ukoloni wakati wa vita baridi, ambao ulilingana na malengo ya sera za kigeni za Urusi. Hii ilisababisha ushirikiano mkubwa kati ya nchi hizo mbili, na msaada wa Urusi ukichangia katika miradi ya maendeleo na jitihada za kiuchumi za Tanzania. Hata hivyo, uhusiano huu haukuwa bila changamoto, kwani msimamo wa kutokujipanga wa Tanzania mara kwa mara uliathiri uhusiano wake na mataifa makubwa yote mawili.

 

Baada ya Vita Baridi kumalizika na Urusi kutokea kama taifa linalofuatia Umoja wa Kisovieti, uhusiano kati ya Urusi na Tanzania ulipitia mabadiliko makubwa. Urafiki wa zamani uliojikita katika misingi ya kiitikadi ulibadilika hatua kwa hatua kuwa ushirikiano wa vitendo zaidi, ukiendeshwa na maslahi ya pamoja.

 

Wakati wa kipindi hiki cha mpito, Urusi na Tanzania ziliadjusti mikakati yao ya kidiplomasia kulingana na mabadiliko katika eneo la kimataifa. Mabadiliko kutoka kwenye maelewano ya kiitikadi hadi ushirikiano wa vitendo yalitokana na haja ya kujenga ushirikiano utakaonufaisha kiuchumi, kisiasa, na kijamii kwa pande zote mbili.

 

Kwa mfano, mataifa yote mawili yalianza kuchunguza fursa za ushirikiano wa kiuchumi, ikiwa ni pamoja na makubaliano ya biashara, fursa za uwekezaji, na miradi ya pamoja katika sekta mbalimbali kama vile uchimbaji madini, nishati, kilimo, na maendeleo ya miundombinu.

 

Wakati nchi hizo mbili zilipoformalize "mahusiano yao" mwaka 1961, mazungumzo na kubadilishana kati ya viongozi wa ngazi za juu yalianza kuchukua nafasi. Uhusiano wa kidiplomasia ulionyesha azma ya kuimarisha uhusiano wa pande mbili na kuchunguza maeneo ya maslahi ya pamoja. Hii ilithibitishwa kwa kuunda kamati ya pamoja ili kuongeza kasi ya mahusiano katika maeneo ya uwekezaji, biashara, na maendeleo ya kiuchumi kati ya nchi hizo mbili mwaka 2019.

 

Juhudi ziliongezwa zaidi kuboresha mahusiano kati ya watu kwa njia ya kubadilishana tamaduni, scholarship za elimu, na programu za ushirikiano katika maeneo kama vile sayansi, teknolojia, na ujenzi wa uwezo kati ya nchi hizo mbili. Hili lilidhihirika wakati wa Julai 2023 wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipotembelea Urusi kuhudhuria Mkutano wa Pili wa Kirusi-Afrika uliofanyika St. Petersburg.

 

Mkutano huo uliowaleta pamoja viongozi na wawekezaji kutoka zaidi ya nchi 37 za Afrika na Urusi, ulijadili njia za kusimamisha ushirikiano, na wakati huo huo kubuni mikakati ya kuboresha changamoto za kila nchi binafsi. "Ushiriki wetu katika jukwaa hili ni muhimu sana kwa Tanzania kwani tunaweza kujifunza kuhusu shughuli za nchi nyingine za Kiafrika katika sekta mbalimbali na kupata uzoefu kutoka kwao," alisema Majaliwa.

 

"Harusi" kati ya Urusi na Tanzania ilithibitishwa baada ya nchi hizo mbili kufanya mazungumzo kuhusu Ushirikiano wa Usalama, Utulivu wa Kikanda, na Msaada wa Kibinadamu, wakiahidi kusaidiana katika nyakati ngumu. Ushirikiano huu ulisisitiza azma ya pamoja ya amani na usalama, kukuza mazingira salama kwa nchi zote mbili na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla.

 

Kwa kweli, Urusi na Tanzania wamepiga hatua ndefu na uhusiano wao unaendelea kustawi huku nchi hizi mbili zikiendelea kudumisha uhusiano wa kidiplomasia, hasa katika maeneo kama Biashara, Nishati, Elimu, na Afya.

 

Linapokuja suala la Elimu, Urusi imekuwa ikihimarika katika kutoa scholarship na fursa za mafunzo kwa wanafunzi na wataalamu wa Kitanzania, kuwapa stadi na maarifa yanayochangia maendeleo