Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi, ilitoa amri ya kupigwa mnada nyumba hiyo na kumteua Jesca Massawe, kutoka Kampuni ya Udalali ya MM Auctioneer &Debt Collectors, kutekeleza amri hiyo.
Tukio hilo limetokea, leo, mkoani Dar es Salaam, Jessica, akiripoti Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Mikocheni A, ilipo nyumba hiyo na kisha kubainisha notisi aliyoibandika nyumbani kwa mtoto wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe.