DW imeripoti kuwa, Papa Francis ameyasema haya katika kitabu kipya ambacho dondoo zake zimechapishwa katika gazeti la Corriere della Sera huko Nchini Italia.
Katika kitabu hicho kinachotarajiwa kutolewa rasmi Machi 19, Papa anasema wazo la kujiuzulu ni ndoto kwakuwa hana sababu yoyote ya kumpelekea kufanya hivyo.
Francis mwenye umri wa miaka 87 katika miaka ya hivi karibuni ameripotiwa kuugua mara kadhaa, ambapo amekuwa akitumia kiti cha magurudumu au mkongojo kutembea, amekuwa akiugua mafua mara kwa mara jambo lililompelekea kupunguza maongezi yake mbele ya umma.